Mandhari ya Mistari Chagua mstari, chagua muonekano, upakue kwa 2K.
Yahwe ni mchungaji wangu; sita pungukiwa na kitu. Yeye hunilaza katika majani mabichi; huniongoza kando ya maji matulivu. Yeye huurejesha uhai wangu; huniongoza katika njia iliyo sahihi kwa ajili ya jina lake.
Zaburi 23:1-3
Ethan.Bible Ukubwa
Simu Kompyuta Chapisho Hadithi
Mtindo
Classic Gold Modern Editorial Glow Bold Script Minimal
Badilisha mandharinyuma Binafsisha Unajisikiaje leo? 😟 Anxious 💔 Grieving 😮💨 Weary 🌙 Lonely 😨 Afraid Overwhelmed 🙏 Grateful 🌅 Hopeful 🕊️ At peace Hisia zaidi (20)
Basi amani ya Bwana iliyo kuu kuliko ufahamu wote, italinda mioyo na mawazo yenu kwa msaad Kristo Yesu. Wafilipi 4:7 Lakini nitaimba kuhusu nguvu zako, na asubuhi nitaimba kuhusu upendo wako imara! maana umekuwa mnara wangu mrefu na kimbilio la usalama katika siku ya taabu. Zaburi 59:16 Kwa hiyo, vaeni silaha zote za Mungu, ili mpate kusimama imara dhidi ya uovu katika kipindi hiki kiovu. Baada ya kumaliza kila kitu, mtasimama imara. Waefeso 6:13 Kama wateule wa Mungu, watakatifu na wapendwao, jivikeni utu wema, ukarimu, unyenyekevu, upole na uvumilivu. Wakolosai 3:12 Tazama nasimama katika mlango na kubisha. Yeyote asikiaye sauti yangu na kufungua mlango, nitakuja na kuingia nyumbani kwake, na kula chakula naye na yeye pamoja nami. Ufunuo 3:20 Uache uovu na utende mema. Uitafute amani na kuiendea amani. Zaburi 34:14 Kwa kuwa katika mpendwa wake, tunaukombozi kupitia damu yake, msamaha wa dhambi. Tunalo hili kwa sababu ya utajiri wa neema yake. Waefeso 1:7 Toeni shukurani kwa Yahweh, kwa kuwa ni mwema, uaminifu wa agano lake la dumu ata milele. 1 Mambo ya Nyakati 16:34 Kwa kuwa wawili au watatu wakikusanyika pamoja kwa jina langu, Mimi niko katikati yao. Mathayo 18:20 Piga vita vizuri vya imani. Shikilia uzima wa milele ulioitiwa. Ilikuwa ni kwa sababu hii kwamba ulitoa ushuhuda mbele ya mashahidi wengi kwa kile kilicho chema. 1Timotheo 6:12 Mungu akaibarikia siku ya saba na akaitakasa, kwa sababu katika siku hiyo alipumzika kutoka kwenye kazi yake yote ambayo aliifanya katika uumbaji. Mwanzo 2:3 Yesu akawatazama na kusema, “Kwa wanadamu hilo haliwezekani, lakini kwa Mungu yote yanawezekana.” Mathayo 19:26 Mwenye ukarimu kwa masikini humkopesha Yehova na atalipwa kwa kile alichofanya. Mithali 19:17 Yeyote ajaribuye kuyaokoa maisha yake atayapoteza, lakini yeyote apotezae maisha yake kwa faida yangu, atayaokoa. Luka 9:24 Mungu amewaiteni ninyi, ndugu, kwenye uhuru. Ila msiutumie uhuru wenu kama fursa kwa mwili. Badala yake kwa upendo mhudumiane ninyi kwa ninyi. Wagalatia 5:13 Tafuteni amani na watu wote, na pia utakatifu ambao bila huo hakuna atakayemwona Bwana. Wahebrania 12:14 Mwamini Yahwe daima; maana Yaha, Yahwe, ni mwamba wa milele. Isaya 26:4 Furahini katika ujasiri mlionao kuhusu siku zijazo. Muwe na subira katika matatizo yenu. Mdumu katika kuomba. Warumi 12:12 Wabarikini wale wanao walaani ninyi na waombeeni wale wanaowaonea. Luka 6:28 Ni amani kuwa nitajilaza na kusinzia, kwako pekee, Yahweh, nifanye kuwa salama kabisa. Zaburi 4:8 Kwa sababu sisi tu kazi ya Mungu, tumeumbwa katika Kristo Yesu kutenda matendo mema. Ni matendo haya ambayo Mungu aliyapanga tangu zamani za kale kwa ajili yetu, ili tutembee katika hayo. Waefeso 2:10 Hivyo, jitoeni kwa Mungu. Mpingeni ibilisi na yeye atakimbia kutoka kwenu. Waraka wa Yakobo 4:7 Fikirini kuhusu mambo ya juu, sio kuhusu mambo ya duniani. Wakolosai 3:2 Yahwe yu karibu nao waliovunjika moyo, naye huwaokoa waliogandamizwa rohoni. Zaburi 34:18